.

Chanzo cha picha, Getty Images

Muda wa kusoma: Dakika 2

Chelsea wameibuka kuwa wapinzani watarajiwa wa Newcastle United katika kuwania saini ya mchezaji wa kimataifa wa Uruguay Darwin Nunez. Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 26 amesalia katika orodha ya wachezaji wa akiba katika klabu ya Al-Hilal ya Saudi Arabia inayompendelea mshambuliaji wa Ufaransa Karim Benzema mwenye umri wa miaka 38. (Chronicle Live)

Manchester City wako tayari kulipa £70m – ada ambayo ni rekodi ya dunia kwa beki wa pembeni – ili kumpata mchezaji wa kimataifa wa Uingereza Tino Livramento, 23, kutoka Newcastle United. (TeamTalks)

Mkataba wa beki wa kati wa Ujerumani Nico Schlotterbeck katika klabu ya Borussia Dortmund unamalizika 2027 na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye amekuwa akihusishwa na Liverpool, ni mmoja wapo wa walengwa wakuu wa Real Madrid msimu huu. (Mundo Deportivo – In Spanish)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Sunderland na West Ham wanavutiwa na mshambuliaji wa Mexico Santiago Gimenez, 24, ambaye anaweza kuruhusiwa kuondoka AC Milan. (AS – In Spanish).

Kipa wa Manchester United Altay Bayindir anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo msimu wa joto, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Uturuki mwenye umri wa miaka 27 akitarajiwa kujiunga na klabu ya Besiktas . (Football Insider)

Mshambulizi wa Uingereza Marcus Rashford, 28, amekubali kupunguzwa kwa mshahara wake huku pia akibashiri baadhi ya bonasi katika juhudi za kufanya uhamisho wake wa mkopo kutoka Manchester United kwenda Barcelona kuwa wa kudumu. (TeamTalks)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Crystal Palace itazuia mbinu zozote za Dean Henderson kutoka Tottenham na vilabu vingine. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye amecheza mechi nne za Uingereza, amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Palace chini ya Oliver Glasner. (Football Insider)

Juventus wanaweza kuwa tayari kumuuza kiungo wa kati wa Uholanzi Teun Koopmeiners lakini wanataka angalau euro 30m (£26m) kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye amekuwa akihusishwa na klabu za Galatasaray na Roma. (Tuttosport – in Italy)

Nottingham Forest haina nia ya kutumia chaguo la euro 35m (£31m) kubadilisha uhamisho wa mkopo wa mshambuliaji wa Italia Lorenzo Lucca kutoka Napoli hadi uhamisho wa kudumu. (Niocolo Schira, via Foot Italy)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *