Maiga ameahidi kuwa Mali haitokalia kimya vitendo vya aina hiyo na kuwa italipa kisasi kwa kila ubaya dhidi yake. Ameitolea wito Algeria kuacha kuunga mkono ugaidi wa kimataifa na badala yake ijikite katika kudumisha amani.

Malalamiko ya Mali dhidi ya Algeria mbele ya ICC

Serikali imeshapeleka malalamiko kwa mahakama ya kimataifa ya uhalifu, hatua ambayo Algeria imeitaja kuwa ya aibu.

Tangu mwezi Aprili, utawala wa kijeshi wa Mali umekuwa ukilalamika kuwa Algeria iliidungua droni yake madai ambayo hata hivyo upande wa pili umeyakanusha.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *