Wagombea tiketi ya urais na makamu wa rais kupitia CCM Rais Samia Suluhu Hassan na Dkt. Emmanuel Nchimbi.

Chanzo cha picha, CCM

Maelezo ya picha, Wagombea tiketi ya urais na makamu wa rais kupitia CCM Rais Samia Suluhu Hassan na Dkt. Emmanuel Nchimbi.

    • Author, Na Charles William
    • Nafasi, Mchambuzi

Ni wazi kwamba joto la kisiasa nchini Tanzania sasa limepanda kwenye kiwango cha juu kabisa. Vyama vyote vyenye ushawishi mkubwa kwa wananchi tayari vimetangaza wazi mikakati yake na kuanza kutambulisha wagombea wao kuelekea uchaguzi ambao kampeni zake zinatarajiwa kuanza mwezi Julai na kutamatika Oktoba 2025.

Januari 19, 2025 Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho ndio chama tawala kinachoendesha serikali nchini Tanzania kiliazimia na kumthibitisha Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea wake wa Urais, lakini pia kimemteua na kumthibisha Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwa mgombea wake katika nafasi ya Makamu wa Rais.

Kwa upande wa Urais wa Zanzibar, sehemu ya pili ya Muungano wa Tanzania chama hicho kilitangaza kumteua Rais wa sasa, Dk. Hussein Mwinyi kuwa mgombea wake kwa asilimia 98 ya kura zilizopigwa.

Maamuzi ya mapema

Je, Lissu kuchuana na Rais Samia kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Chanzo cha picha, Ikulu Tanzania

Maelezo ya picha, Je, Lissu kuchuana na Rais Samia kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Hatua ya CCM kufanya uteuzi wa wagombea wake mwezi Januari, haikutarajiwa na wengi na wala haikuwa sehemu ya ajenda zilizotangazwa katika ratiba rasmi ya mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika kwa siku mbili mfululizo, Januari 18 na Januari 19 jijini Dodoma. Kwa kawaida chama hicho huteua wagombea wake kati ya mwezi Mei mpaka Julai katika mwaka wa uchaguzi.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *