d

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Rais wa mpito wa Syria, Ahmed al-Sharaa

Huku kukiwa na misukosuko ya kisiasa nchini Syria, waandishi katika magazeti ya kimataifa wanazidi kujadili upinzani wa ndani wa Syria kuhusu mazungumzo na Israel na ripoti za vyombo vya habari kuhusu mikutano ya siri inayolenga kujadili uwezekano wa makubaliano ya usalama chini ya usimamizi wa Washington.

Tunaanza ziara yetu katika gazeti la Emirati, The National, kwa makala ya mwandishi Raghida Dergham, ambapo anauliza, “Kwa nini Syria ina haki ya kuzungumza na Israel?”

Mwandishi anasema uongozi mpya wa Syria, baada ya “kuifukuza Iran na Hezbollah katika nchi hiyo,” unaongoza mabadiliko katika uhusiano wake wa kikanda, hasa uhusiano wake na Israel.

Dargham anaeleza kwamba Syria, ambayo hapo awali ilikuwa “nguzo ya mradi wa upanuzi wa Iran,” sasa inatafuta kujiweka upya kikanda na kimataifa. Mabadiliko haya, anasema, yanafanyika kwa usaidizi wa nchi za Ghuba na ufadhili wa Marekani, chini ya uongozi mpya wa Syria unaowakilishwa na rais wa mpito Ahmed al-Sharaa.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *