s

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Emiliano Martinez

Aston Villa hawakupokea ofa kutoka Manchester United kwa ajili ya kipa wa Argentina Emiliano Martinez licha ya mchezaji huyo mwenye miaka 32 kuhusishwa sana na uhamisho wa kuelekea Old Trafford. (Sky Sports)

Manchester United waliamua kutomchukua Martinez kwa sababu ya umri wake na mshahara unaokaribia pauni 200,000 kwa wiki. (Mirror)

Martinez hakuwa na hamu ya kujiunga na Galatasaray licha ya ripoti kutoka Uturuki kuhusu ofa ya thamani ya pauni milioni 21.6. (Daily Mail)

Liverpool walikataa kumruhusu Joe Gomez, 28, kujiunga na AC Milan baada ya mpango wao wa kumsajili beki wa England Marc Guehi, 25, kutoka Crystal Palace kuvunjika. (Fabrizio Romano)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *