Picha ya wanaume wawili waliovaa sare za kijeshi wakionyeshana mgongo wao huku kando ya picha hiyo ni mchoro wa bendera

Chanzo cha picha, Raees Hussain / BBC, Getty

Maelezo ya picha, Picha ya wanaume wawili waliovaa sare za kijeshi wakionyeshana mgongo wao huku kando ya picha hiyo ni mchoro wa bendera

    • Author, Cagil Kasapoglu
    • Nafasi, BBC World Service

Kati ya Lithuania na Poland kuna mkanda mdogo wa ardhi unaojulikana kama Suwałki Gap, ambao mara nyingi hufafanuliwa na wachambuzi wa kijeshi kuwa ndio eneo dhaifu zaidi la NATO maarufu pia kama “eneo la hatari”.

Iwapo mzozo wa kijeshi ungefumuka kati ya NATO na Urusi, ushoroba huu mwembamba ungewakilisha kitovu cha mivutano ya kijeshi.

Wasiwasi mkubwa ni kwamba iwapo Urusi, kwa kushirikiana na mshirika wake Belarusi, ingeuteka au kuufunga ushoroba huu, ingeweza kuyatenga mataifa ya Baltiki – Lithuania, Latvia na Estonia – kutoka kwa washirika wao wa NATO barani Ulaya.

Mnamo Juni 2025, Mkuu wa Majeshi wa Ujerumani, Jenerali Carsten Breuer, aliwaambia waandishi wa habari wa BBC kuwa nchi wanachama wa NATO lazima zijiandae kwa uwezekano wa shambulio la Urusi ndani ya kipindi cha miaka minne ijayo.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *