Baraza hilo lenye wanachama 193 lilimchagua mwanasiasa huyo wa Kikurdi mwenye umri wa miaka 65 kuwa kamishna mkuu wa UNHCR kwa makubaliano na Rais wa Baraza Kuu Annalena Baerbock.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, amemsifu kiongozi huyo kutokana na uzoefu wake kwenye eneo la diplomasia, siasa na utawala na kumtaja kama mbunifu wa mageuzi ya kitaifa.

Salih anachukua nafasi ya Filippo Grandiambaye muda wake wa awamu ya pili unamalizika Disemba 31. Kipindi cha Salih kitaanza Januari Mosi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *