,

Chanzo cha picha, Reuters

Watoto 130
wa shule wa Nigeria waliokuwa bado wametekwa nyara kutokana na uvamizi wa mwezi
Novemba kutoka shule ya Kikatoliki katika jimbo la Niger wameachiliwa huru,
msemaji wa Rais Bola Tinubu alisema Jumapili, kufuatia moja ya utekaji nyara
mkubwa zaidi nchini humo katika miaka ya hivi karibuni.

“Watoto
130 waliokuwa bado wametekwa nyara na watekaji…sasa wameachiliwa huru.
Wanatarajiwa kufika Minna Jumatatu na kuungana na wazazi wao kwa sherehe ya
Krismasi,” Bayo Onanuga alisema katika chapisho kwenye mtandao wa X.

“Kuachiliwa
huru kwa watoto wa shule kumewezeshwa na operesheni iliyoendeshwa na ujasusi wa
kijeshi.”

Wanafunzi
hao ni miongoni mwa zaidi ya wanafunzi 300 na wafanyakazi 12 waliokamatwa na
watu wenye silaha kutoka shule ya bweni ya St Mary’s Catholic katika kijiji cha
Papiri saa za mapema Novemba 21.

Watoto hamsini
kati ya watoto hao walifanikiwa kutoroka wakati huo, Chama cha Wakristo cha
Nigeria kilisema hapo awali, huku serikali ya Nigeria ikisema mnamo Desemba 8
kwamba ilifanikiwa kuwaokoa 100 kati ya waliotekwa nyara.

Onanuga
alisema jumla ya wanafunzi walioachiliwa huru sasa ni 230.

Utekaji
nyara huo ulisababisha hasira juu ya kuongezeka kwa ukosefu wa usalama
kaskazini mwa Nigeria, ambapo magenge yenye silaha mara nyingi hulenga shule
kwa ajili ya kulipwa fidia. Utekaji nyara shuleni uliongezeka baada ya
wanamgambo wa Boko Haram kuwateka nyara wasichana 276 kutoka Chibok mwaka wa
2014.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *