
Inatarajiwa kwamba kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki atazungumza dhidi ya vita na vurugu, na kukumbuka mateso ya binadamu.
Papa Leo tayari ametoa matamko kadhaa akitoa wito wa amani na upatanisho, na kuwakumbuka waathiriwa wa vita duniani kote.
Baba Mtakatifu Leo amesema anarejea ombi lake kwa watu wote wenye nia njema kuifanya Krismasi kuwa siku ya amani, kwa angalau kuonesha heshima kwa siku hiyo ya kuzaliwa Yesu Kristo.
Wakristo duniani watasherehekea sikukuu ya Krismasi hapo kesho kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu zaidi miaka 2000 iliyopita.