Papa Leo ameelezea masikitiko yake baada ya ombi la kusitisha mapigano kwa alau kwa muda mfupi kukataliwa na na Urusi, ikizingatiwa ongezeko la mashambulizi makubwa ya hivi karibuni dhidi ya Ukraine.
Kiongozi huyo wa kiroho ambaye alianza kuhudumu mwezi Mei, ataongoza Misa yake ya kwanza ya Krismasi usiku wa leo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, ambako anatarajiwa kulaani vita na vurugu na kukumbusha mateso ya raia.
Katika tamko lake la awali , Papa Leo alizungumzia hali ya Mashariki ya Kati, akisema wakaazi wa eneo hilo wanajaribu kusherehekea Krisimasi licha ya mazingira magumu.
