
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza siku ya Jumapili, Desemba 28, kwamba alikuwa “karibu sana” na makubaliano kuhusu mpango wa amani kwa Ukraine kufuatia mkutano na mwenzake wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, ambaye alimmpokea huko Florida, ingawa viongozi wote wawili walikiri kwamba baadhi ya ponti ngumu bado zinasalia kutatuliwa.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Donald Trump alisema siku ya Jumapili, wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika makazi yake ya Florida pamoja na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, kwamba “maendeleo mengi” yamefanywa kuelekea “kukomesha vita” kati ya Ukraine na Urusi wakati wa mkutano wake na mwenzake wa Ukraine, huku akikiri kwamba “sehemu moja au mbili ngumu” sinasalia kutatuliwa. Rais wa Marekani pia alikiri kwamba masuala ya maeneo yanayoshikiliwa na Urusi bado hayajatatuliwa. “Tunakaribia sana, labda hata karibu sana,” makubaliano kuhusu Donbas, Donald Trump ameongeza.
Donald Trump amebainisha kwamba hitimisho la mazungumzo kuhusu makubaliano ya amani kati ya Ukraine na Urusi linaweza kujulikana katika wiki zijazo. “Nadhani katika wiki chache zijazo, tutajua kwa njia moja au nyingine” kama mazungumzo yamefanikiwa, na kuongeza kwamba mazungumzo yalikuwa “magumu sana.”
Alipoulizwa kuhusu ziara inayowezekana nchini Ukraine, Donald Trump hakukataa, akisema: “Nimejitolea kwenda huko na kuzungumza mbele ya Bunge lao.”
Hakuna “tarehe ya mwisho” zaidi ya “kumalizika kwa vita”
Ingawa Volodymyr Zelensky alitangaza kwamba makubaliano yamefikiwa kuhusu dhamana za usalama ambazo zingetolewa kwa Ukraine kama sehemu ya mpango wa amani na Urusi, Donald Trump alikuwa mwangalifu zaidi, akisema kwamba suala hilo “limetatuliwa kwa asilimia 95.” Pia alisema alitarajia nchi za Ulaya kuchukua “sehemu kubwa” ya dhamana hizi za usalama, kwa usaidizi wa Marekani.
Kama kawaida anapozungumzia suala la Ukraine, rais wa Marekani anatoa sauti ya matumaini, bila kutoa maelezo yoyote halisi kuhusu maendeleo anayotaja, anaripoti mwandishi wetu huko New York, Loubna Anaki. Kwa kweli, majadiliano yanayozunguka mpango wa amani ni magumu, hasa kuhusu suala la Donbas, ambalo linabaki kuwa moja ya hoja kuu za mzozo, kama Volodymyr Zelensky alivyoelezea. “Lazima tuheshimu sheria zetu na watu wetu kuhusu hatima ya eneo tunalolidhibiti. Ndiyo maana Rais Trump anasema ni suala gumu. Tuna msimamo tofauti sana na Urusi kuhusu jambo hili.” Rais wa Ukraine alithibitisha tena kwamba uamuzi wowote muhimu kwa nchi lazima uwasilishwe kwa kura ya maoni au kuidhinishwa na bunge.
“Wiki kadhaa zaidi za majadiliano zinatarajiwa”
Wawili hao walikiri kwamba huenda itachukua wiki kadhaa kufikia makubaliano yoyote ya amani. Lakini waliahidi kuendelea na mazungumzo. “Pande zote zinahitaji amani,” Donald Trump alibainisha. “Ukraine inataka amani, Urusi inataka amani,” alisema.