Viongozi wa Hamas

Vita vilivyoanza kati ya Israel, Hamas, na makundi mengine ya Wapalestina yenye silaha katika Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 7, 2023, ni sehemu moja tu ya mfululizo unaoendelea wa makabiliano, ghasia, mauaji, na mashambulizi ya kujitoa mhanga tangu kuanzishwa kwa Harakati ya Upinzani ya Kiislamu, inayojulikana kama Hamas, mnamo 1987 na marehemu Mpalestina, Ahmed Yassin.

Vuguvugu hilo lilianzisha makumi ya mashambulizi ya kujitoa muhanga ndani ya Israel, na kuua mamia ya Waisraeli, wakati wa Intifada ya Kwanza, iliyoanza katika Ukanda wa Gaza mwaka 1987 ilipokuwa chini ya utawala wa Israel. Ilienea hadi Ukingo wa Magharibi na kumalizika kwa kusainiwa kwa Makubaliano ya Oslo mnamo 1993.

Intifadha ya Pili, ambayo ilizuka baada ya kiongozi wa upinzani wa wakati huo wa Israel, Ariel Sharon kuingia Msikiti wa Al-Aqsa mwaka 2000, ilikuwa na umwagaji damu na vurugu zaidi kuliko Intifadha ya Kwanza, ambapo watu 4,200 waliuawa kwa pande zote mbili, kiwango cha Muisraeli mmoja kuuawa kwa kila Wapalestina watatu.

Israel imefanya mauaji kadhaa yakiwalenga viongozi wa kundi la Wapalestina, shambulizi la hivi punde zaidi likiwa ni shambulio la anga kwenye mji mkuu wa Qatar, Doha, Septemba 9. Israel ilijaribu kuwauwa viongozi wa Hamas huko Doha, lakini Hamas ilitangaza kuwa jaribio hilo “lilishindwa.”



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *