Katika zama hizi za kidijitali, taasi­si, mashirika na vyama vya wafanya­kazi kote ulimwenguni vinaendelea kubadilisha njia za kufanya kazi ili kukidhi mahitaji ya wanachama, kuongeza ufanisi na kufikia malengo ya kitaasisi na kijamii kwa kutumia teknolojia.

Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fed­ha Huduma na Ushauri (TUICO) ni miongoni mwa taasisi ambazo zimeanza safari ya nguvu kuelekea uwekezaji wa kidijitali na matumizi ya teknolojia ili kuboresha huduma kwa wanachama wake na kushiriki­ana vyema katika sekta zinazobadi­lika kwa kasi.

Wakati inapoadhimisha mia­ka 30 tangu kuanzishwa kwake, TUICO imepiga hatua kubwa kati­ka matumizi ya teknolojia husu­sani katika shughuli za kila siku. Mawasiliano, usajili wa wanachama na usimamizi wa taarifa za wana­chama umekuwa ni wa kidijitali. Mabadiliko haya yanaonyesha jiti­hada za chama kwenda na wakati pia ikihakikisha majukumu ya kum­tetea na kumlinda mfanyakazi yana­fanyika kwa ufanisi.

Hapo awali, upatikanaji na utoaji wa taarifa ulitegemea nyaraka za karatasi. Hili lilichangia upotevu wa taarifa na matumizi ya muda mre­fu kupata taarifa muhimu kwenye ngazi mbalimbali za Chama. Hivyo chama kikaanza matumizi ya mifu­mo ya kiteknolojia ili kutatua chan­gamoto hii.

Mabadiliko makubwa yalianza mwaka 2017 kwa kuanzishwa kwa tovuti ya chama ambayo ilitambu­lisha uwepo wa TUICO mtandaoni na kutoa nafasi kwa wanachama na umma kupata taarifa kuhusu chama na shughuli zake bila kufika kwenye ofisi za mikoa au makao makuu ya chama. Uwepo huu mtandaoni uliimarishwa zaidi baada ya kuan­zishwa kwa kurasa rasmi za mitan­dao ya kijamii.

Hili liliwezesha mawasiliano ya haraka zaidi na kurahisisha upatika­naji wa taarifa. Pamoja na mabore­sho haya, TUICO ili kuongeza ufani­si wa utendaji katika kusajili na kutunza taarifa za wanachama kwa kuanzisha Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa (MIS), ambalo ni mfumo wa kidijitali wa usimamizi wa taarifa za wanachama.

Kabla ya TUICO-MIS, kupata taar­ifa za mwanachama, kuthibitisha uanachama au kusahihisha taarifa kulichukua muda mrefu na ilikuwa ngumu. Lakini kwa sasa inaweze­kana kwa dakika chache. Hili lim­eongeza ufanisi mkubwa kwani kazi hiyohiyo hapo awali ilitumia masaa mengi.

Aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe Ridhiwani Kikwete (katikati, walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi wakati wa uzinduzi wa miongozo ya mifumo ya kielektroniki na majadiliano ya Serikali na vyama vya wafanyakazi na waajiri. TUICO ni moja ya vyama vilivyoshiriki uzinduzi huo uliofanyika Agosti mwaka huu.

Kwa kuwa ofisi zote zinatumia MIS, taarifa kutoka tawi lolote zinafikiwa mara moja katika ofisi ya mkoa na Makao Makuu kwa haraka na kwa wakati. Pia ripoti ambazo hapo awali zingechukua siku kuandaliwa sasa zinaweza kuandaliwa kwa dakika chache, hili limepelekea kuboresha upan­gaji, uratibu, na uwajibikaji. Hivyo matumizi ya teknolojia yaameba­dilisha jinsi TUICO inavyosimamia taarifa za wanachama, na kufanya huduma kutolewa kwa haraka.

TUICO haijaishia kwenye kuan­zisha na kutumia mifumo ya kidi­jitali pekee. Chama kimeendelea kuwajengea uwezo watendaji wake kote nchini jinsi ya kutumia mifumo na vifaa vya kidijitali kwa ufanisi, ili kuhakikisha kila mmoja anaweza kutoa huduma na kusi­mamia taarifa za wanachama kwa urahisi.

Wakati huo huo, TUICO pia imewekeza katika vifaa vya kisasa kama kompyuta, kompyuta mpa­kato (Laptop) na zana nyingine pamoja na kuunganisha mtandao (internet) kwenye ofisi zake zote ili kuendana na mabadiliko ya kitenolojia.

Hatua hizi zinahakikisha matumizi ya mifumo ya cha­ma unaendelea kuimarika huku uwezo wa wafanyakazi, kufanya kazi kwa ufanisi unaongezeka na kuhakikisha wanachama wanapa­ta huduma kwa wakati.

Kutokana na mapinduzi ya kidijitali Tanzania kuendelea kwa kasi ikiwa ni pamoja na ongeze­ko la watumiaji wa intaneti na matumizi ya huduma za 5G na huduma za Serikali mtanda­oni, TUICO inaendelea kupanua uwekezaji wake wa teknolojia na kuboresha huduma kwa wanacha­ma

TUICO imeanza safari muhimu ya uwekezaji wa kidijitali na matumizi ya teknolojia, kuwekeza zaidi kwenye mifumo ya TEHA­MA, kutumia majukwaa ya mtand­ao na mitandao ya kijamii, kusima­mia taarifa kwa njia ya kidijitali, kuhamasisha elimu ya teknolojia kwa wanachama na kuchangia kwenye mabadiliko ya kijamii.

Kwa kuendelea kuboresha rasilimali hizi, chama kinajiweka katika mstari wa mbele wa vyama vya kisasa vinavyotumia tekno­lojia kukuza haki za wafanyakazi na ushiriki wa wanachama katika zama za digitali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *