Maafisa wa Palestina wamesema karibu watu 20 wakiwemo waandishi wa habari watano, waliuawa kwenye shambulizi la Israel kwenye Hospitali ya Nasser.

Mkuu wa idara hiyo ya mawasiliano Burhanettin Duran ameandika kwenye mtandao wa X kwamba Israel inayoendeleza mauaji holela bila ya kujali utu ama misingi ya kisheria, inajidanganya kwamba itazuia ukweli kufichuliwa kwa kuwashambulia wanahabari.

Jeshi la Israel limekiri kufanya shambulizi hilo na kusema tayari mkuu wa utumishi ameagiza uchunguzi na kuongeza kuwa linajutia madhara yoyote dhidi ya watu ambao hawakuhusika, na kusema haliwalengi waandishi wa habari.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *