FV

Chanzo cha picha, MITANDAO

Mbio za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 zinazidi kushika kasi. Ni uchaguzi ambao Watanzania watamchagua rais wa Jamhuri ya Muugano, wabunge, madiwani na upande wa Zanzibar, watachagua rais, wawakilishi na nafasi sawa na za Tanzania bara.

Huu ni uchaguzi wa saba tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Lakini ndio wa kwanza kwa chama tawala CCM, kuweka mgombea mwanamke, ambaye anatarajiwa kuwa rais wa sasa Samia Suluhu Hassan.

Tangu Bunge la 12 la Tanzania kukamilisha rasmi shughuli zake tarehe 27 Juni 2025. Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, kumesheheni picha za watia nia hasa katika nafasi ya Ubunge – na watia nia wengi wanaonekana kuelekea chama tawala.

Watia nia wako makundi mawili; wale ambao wamezoeleka kuonekana katika shughuli za kila siku za Chama cha Mapinduzi (CCM), na hakuna anayefumbua mdomo akisikia wanataka kugombea ubunge. Kundi la pili, ni watia nia ambao hawana kabisa historia ya kujishughulisha na shughuli za wazi za CCM.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *