Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amenukuliwa na televisheni ya taifa akisema hakuna makubaliano ya mwisho yaliyofikiwa kuhusu mfumo mpya wa ushirkiano na Shirika la Kudhibiti Nguvu za Atomiki duniani, IAEA na kwamba bado wanabadilishana maoni.

Mazungumzo ya nyuklia ya Iran yakamilika bila mafanikio

Kwa upande wake, msemaji wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran, Behrouz Kamalvandi, amesema wakaguzi hao wa IAEA watasimamia ubadilishaji wa mafuta katika kinu cha nyukliacha Bushehr kusini magharibi mwa nchi hiyo.

Hata hivyo, hakusema kama wakaguzi hao wataruhusiwa kufika maeneo mengine ya vinu vya nyuklia, ikiwa ni pamoja na Fordo na Natanz, ambavyo vililengwa wakati wa vita.

Kurejea kwa wakaguzi hao kumekuja baada ya wanadiplomasia wa Irankufanya mazungumzo na wenzao kutoka Uingereza, Ufaransa na Ujerumani hapo jana mjini Geneva.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *