Alexander Isak

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Alexander Isak

Mshambuliaji wa Sweden Alexander Isak, mwenye umri wa miaka 25, ameiambia Newcastle kwamba bado anataka kuondoka na kujiunga na Liverpool licha ya jitihada za mwenyekiti wa klabu Yasir Al-Rumayyan na kikao na mmoja wa wamiliki wenza Jamie Reuben. (Telegraph)

Manchester United imefikia makubaliano ya awali na Real Betis kwa ajili ya winga wa Kibrazili Antony, 25, kurejea katika klabu hiyo ya Hispania kwa mkopo wenye sharti la kununuliwa moja kwa moja. (Telegraph)

Manchester United pia inatarajia kukubaliana masharti binafsi na kipa Senne Lammens ili kumsajili mchezaji huyo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 23 kutoka Royal Antwerp kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Telegraph)

Real Madrid na Atletico Madrid wanamfuatilia kiungo wa timu ya taifa ya Uingereza Kobbie Mainoo, 20, wa Manchester United ambaye anataka kuondoka baada ya kukosa nafasi kwenye kikosi cha Old Trafford. (Mail)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *