Carolyne Odour's sons - 12-year-old Daniel on the right in a yellow T-shirt and on the left, nine-year-old Elijah. They are standing outside in front of a window with a white curtain drawn.

Chanzo cha picha, Carolyne Odour

Maelezo ya picha, Elijah, mwenye umri wa miaka tisa, na Daniel, mwenye umri wa miaka 12, walitoweka baada ya kuondoka kwa basi mnamo 28 Juni

    • Author, Anita Nkonge
    • Nafasi, BBC News Nairobi

Carolyne Odour ameiambia BBC kuwa anahofia sana hatima ya wanawe wawili wadogo ambao walitoweka miezi miwili iliyopita na baba yao – mfuasi wa mafundisho ya kiongozi mashuhuri wa ibada ya njaa.

Bi Odour anasema kuwa huku kukiwa na uchunguzi unaoendelea kuhusu vifo zaidi vinavyohusiana na ibada hiyo ameutambua mwili wa mumewe katika chumba cha kuhifadhia maiti mjini Malindi pwani ya Kenya.

Maiti yake ilipatikana mnamo mwezi wa Julai katika kijiji cha Kwa Binzaro, viungani mwa Malindi na karibu na msitu wa Shakahola, ambapo zaidi ya miili 400 ilipatikana mnamo 2023 katika mojawapo ya visa vibaya zaidi kuwahi kutokea vya vifo vya watu wengi vinavyohusiana na ibada.

Bi Odour sasa anasubiri matokeo ya vipimo vya viini vya vinasaba yaani DNA vinavyofanywa kwa zaidi ya miili 30 iliyogunduliwa hivi karibuni.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *