[ad_1]

fcv

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Vilabu vya Ligi Kuu England vimetumia fedha nyingi kuliko wakati wowote ule kwenye dirisha moja la usajili, baada ya matumizi ya dirisha hili la kiangazi lililofungwa usiku wa jana kuvuka pauni bilioni 3.

Jumla ya pauni bilioni 2.73 zilikuwa zimetumika hadi kufikia tarehe 31 Agosti, lakini usajili wa dakika za mwisho ukiongozwa na usajili wa Alexander Isak kutoka Newcastle kwenda Liverpool kwa ada ya rekodi ya Uingereza ya pauni milioni 125, zimefanya jumla ya matumizi kufikia pauni bilioni 3.087.

Matumizi haya ni makubwa zaidi ikilinganishwa na dirisha la kiangazi lililopita, ambapo vilabu vya ligi kuu vilitumia pauni bilioni 1.96 pekee.

Kiwango cha matumizi katika dirisha hili pia ni kikukubwa zaidi kuliko matumizi yote ya usajili katika ligi ya ujerumani (Bundesliga), Hispania (La Liga), Ufaransa (Ligue 1) na Italia (Serie A).

[ad_2]

Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *