Clarke Oduor ndiye mchezaji pekee wa Grimsby kukosa penalti katika ushindi wao wa mikwaju 12-11 dhidi ya Manchester United

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Clarke Oduor ndiye mchezaji pekee wa Grimsby kukosa penalti katika ushindi wao wa mikwaju 12-11 dhidi ya Manchester United

    • Author, Mariam Mjahid
    • Nafasi, BBC Swahili

Klabu ya Grimsby Town imejikuta matatani licha ya ushindi wao mkubwa kwenye Kombe la Carabao wiki jana baada ya kutozwa faini ya pauni 20,000 kwa kumchezesha mchezaji aliyekuwa hajakamilisha usajili kwa wakati.

Katika mechi hiyo ya kusisimua, Grimsby waliibuka na ushindi dhidi ya Manchester United kwa njia ya mikwaju ya penalti, baada ya sare ya mabao 2-2 ndani ya dakika 90.

Lakini furaha yao imeingia doa kufuatia makosa ya kiufundi wakati wa usajili.

Clarke Oduor ambaye ni raia wa Kenya, kiungo aliyesajiliwa kwa mkopo kutoka Bradford City, alichezwa kama mchezaji wa akiba lakini baadaye ilibainika kuwa jina lake liliwasilishwa kwa EFL dakika moja na sekunde 59 baada ya muda wa mwisho wa saa 6:00 mchana (BST).



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *