Anderson

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

Manchester United inataka kumsajili kiungo wa kati wa Nottingham Forest na England mwezi Januari Elliot Anderson, 22. (Teamtalk)

Arsenal imepiga hatua katika mazungumzo ya kurefusha mikataba ya winga wa Uingereza Bukayo Saka,24, na beki wa Ufaransa William Saliba,24, mikataba hiyo itakapomalizika mwishoni mwa msimu wa 2026-27. (Teamtalk)

Kipa wa Cameroon Andre Onana, ambaye anakaribia kujiunga na Trabzonspor ya Uturuki kwa mkopo, alikataa ofa kutoka kwa vilabu kadhaa – ikiwa ni pamoja na Monaco – msimu wa kiangazi baada ya mchezaji huyo wa miaka 29 kuambiwa atakuwa chaguo la kwanza la kocha wa Manchester United Ruben Amorim msimu huu. (The i Paper – Usajili unahitajika)

Beki wa Manchester United na Uholanzi Tyrell Malacia, 26, anaweza kutolewa mkopo wa msimu mzima katika klabu ya Uturuki ya Super Lig Eyupspor. (Sun)



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *