Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal imempa beki wa Ufaransa William Saliba nyongeza ya kandarasi ya miaka mitano huku ikiendelea kujadiliana na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, ambaye mkataba wake wa sasa unakamilika 2027. Real Madrid wanafuatilia hali ya beki huyo wa kati. (FootMercato – kwa Kifaransa)
Liverpool ina imani kuwa inaongoza katika mbio za kumsajili beki wa Uingereza Marc Guehi, 25, msimu ujao wa kiangazi wakati mkataba wa beki huyo wa Crystal Palace utakapokamilika na wanaandaa dau la la pauni milioni 87 kumsaini winga wa Bayern Munich na Ufaransa Michael Olise, 23. (Caught Offside)
Mgombea urais wa Benfica Joao Noronha Lopes anataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Manchester City Bernardo Silva mwezi Januari endapo atachaguliwa na tayari amefanya mazungumzo na mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 31, ambaye mkataba wake utamalizika msimu ujao. (Record – kwa Kireno)
Manchester United inawakagua mabeki wa Uingereza Harry Maguire, 32, na Luke Shaw, 30, wakati ikijiandaa kuimarisha safu yake ya ulinzi msimu ujao. (Teamtalk)
Besiktas wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili winga wa Ureno Jota Silva, 26, kutoka Nottingham Forest. (Fabrizio Romano)
Winga wa Colombia Luis Diaz, 28, alitaka kuondoka Liverpool msimu uliopita na The Reds ilipendekeza wabadilishane na mshambuliaji wa Manchester City Julian Alvarez, 25, lakini Muargentina huyo alijiunga na Atletico Madrid, wakati Diaz sasa yuko Bayern Munich. (Telegraph – usajili unahitajika)
Chanzo cha picha, Getty Images
Martial atasafiri hadi Monterrey kwa uchunguzi wa afya baada ya kupewa ruhusa ya kufanya hivyo na klabu ya AEK Athens. (Fabrizio Romano)
Juventus inamfuatilia mshambuliaji wa Atalanta Ademola Lookman mwenye umri wa miaka 27 na anayeongoza orodha ya wachezaji wanaopigiwa upatu kumrithi Dusan Vlahovic wa Serbia, 25, ambaye anatarajiwa kuondoka katika klabu hiyo ya Serie A. Mshambuliaji wa Manchester United na Uholanzi Joshua Zirkzee, 24, ni miongoni mwa wanaolengwa. (Tuttosport – kwa Kiitaliano)
Inter Milan bado wanavutiwa na kiungo wa kati wa Ufaransa Manu Kone na nia yao ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 inachochewa na hitaji la Roma kutafuta pesa kutimiza sheria za matumizi ta fedha. (Gazzetta dello Sport – kwa Kiitaliano)
Kiungo wa kati wa Chelsea na Ureno Dario Essugo mwenye umri wa miaka 20 amefanyiwa upasuaji wa jeraha la paja na anaweza kuwa nje kwa muda usiopungua wiki 12. (Usajili unahitajika)