
Baraza la Katiba la Cameroon siku ya Jumatatu, Oktoba 27 limetangaza ushindi wa Paul Biya, rais aliye madarakani, katika uchaguzi wa rais uliofanyika moja iliyopita. Huko Douala, mji mkuu wa kiuchumi ambapo maandamano yalisababisha vifo vya watu wanne siku ya Jumapili, hali imekuwa ya wasiwasi tangu matokeo yatangazwe. Mtaa wa New Bell umekuwa chini ya amri ya kutotoka nje kwa saa kadhaa.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Vikosi vya usalama kwa sasa vinajaribu kutawanya kundi la kwanza la waandamanaji katika mtaa huo, haswa kwa kutumia gesi ya machozi, anaripoti mwandishi wetu huko Douala, Richard Onanena. Tangu kutangazwa kwa ushindi wa Paul Biya kwa muhula wa nane, mvutano umeongezeka baada ya ùakundi ya kwanza ya vijana kuvamia mitaa ya mtaa huo.
Mtaa wa New Bell sasa uko chini ya amri ya kutotoka nje. Jeshi na polisi wanazuia watu kuingia na kutoka katika baadhi ya mitaa katika eneo hilo, na ving’ora husikika mara kwa mara. Polisi na askari pia wanashika doria wakizunguka mitaa ya eneo hilo, na kufanya kuwa vigumu kwa madereva, haswa waendesha pikipiki za kukodiwa, kufanya shughuli zao.
Mvutano pia unaongezeka Garoua
Mvutano pia unaongezeka katika vitongoji kadhaa vya jiji hilo, kama vile Bessingue, ambapo makundi ya vijana pia wanaanza kuikusanya. Kwa ujumla, jiji hili lilikuwa shwari kiasi asubuhi ya Jumatatu, lakini ikumbukwe kwamba shule na maduka makubwa kadhaa yamefungwa.
Mvutano pia unaripotiwa Garoua, ambapo mpinzani mkuu wa Paul Biya, Issa Tchiroma Bakary, yuko. Makabiliano yameripotiwa Marouaré, karibu na makazi ya kiongozi wa upinzani. Amekuwa akijificha huko tangu Oktoba 12 baada ya kupiga kura, akilindwa na kundi la wafuasi wake vijana.
Makabiliano kati ya waandamanaji na vikosi vya usalama yanaendelea, na vyombo vya habari vya ndani vinaripoti kusikika kwa milio ya risasi. Makabiliano pia yameripotiwa nyumbani kwa Yerima Dewa, makamu wa rais wa zamani na jirani wa Issa Tchiroma Bakary. Waandamanaji wametawanywa na vikosi vya usalama.
Umoja wa Mataifa wataka pande zinazokinzana “kujizuia” na kuanzisha uchunguzi
Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa imetoa wito wa uchunguzi kufuatia ripoti za vurugu zinazohusiana na uchaguzi wa urais nchini Cameroon.
“Tangu jana [Jumapili], tumekuwa tukipokea ripoti za kushtua za watu waliouawa, kujeruhiwa, au kukamatwa wakati wa maandamano yanayohusiana na tangazo la leo [Jumatatu] la matokeo ya uchaguzi wa urais. Tunatoa wito wa pande zinazikinzana kujizuia, kufunguliwa kwa uchunguzi, na kukomeshwa kwa vurugu,” Ofisi ya Kamishna Mkuu imesema kwenye mtandao wa kijamii wa X.