
Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov, leo ameyaambia mashirika ya habari ya Urusi
kwamba Ukraine imekataa pendekezo la Urusi la kuitaka kuruhusu waandishi wa habari wa nchi za Magharibi kutembelea eneo hilo, licha ya hamu yao kubwa.
Peskov alihoji kuhusu kinachofichwa Kiev akielezea hali ya kukata tamaa kwa wanajeshi wa Ukraine.
Mara kwa mara, jeshi la Ukraine limekanusha madai ya Urusi ya kuzingira eneo hilo.
Putin aishauri Ukraine
Rais wa Urusi Vladimir Putin ameutaka uongozi wa Ukraine kufanya maamuzi kwa maslahi ya wananchi na wanajeshi wake, akimaanisha kuzingirwa kwa Pokrovsk na Kupiansk katika mkoa wa Kharkiv.
Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema vikosi vyake huko Pokrovsk vitaendelea kuviangamiza vikosi vya Ukraine vilivyozingirwa, huku vikizuia mashambulizi kutoka Kiev.