Kupitia chapisho kwenye mtandao wa X, Chikli amesema mji huo ambao awali ulikuwa ishara ya uhuru wa kimataifa umekabidhi funguo zake kwa wafuasi wa Hamas.

Chikli pia amesema New York haitakuwa tena kama ilivyokuwa awali hasa kwa jamii ya Kiyahudi na akaongeza kuwa jiji hilo linajitumbukiza wazi ndani ya shimo ambalo Uingereza tayari imejiingiza.

Ameendelea kusema kwamba maoni ya Mamdani hayatofautiani pakubwa na yale ya wafuasi wa itikadi kali ambao, miaka 25 iliyopita, waliwaua watu elfu tatu, akimaanisha mashambulizi ya Septemba 11, 2001 yaliofanywa na kundi la Al-Qaeda huko New York na Washington.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *