Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumatatu, aliongoza adhimisho la miaka 87 ya kifo cha Mustafa Kemal Ataturk, baba wa taifa na mwanzilishi wa jamhuri ya Uturuki.

Akizungumza wakati wa adhimisho hilo, Erdogan alimuenzi Ataturk, akiwashukuru wanachama wa kwanza wa Bunge la Taifa, ambao waliongoza mapambano ya uhuru na uanzishwaji wa dola mpya ya Uturuki.

Pia, alitoa heshima kwenye kumbukumbu ya mashahidi wa taifa—wakiwemo wale wa ukombozi wa Istanbul na mapambano ya Canakkale na mashujaa wa Julai 15 ambao walizima jaribio la mapinduzi.

Akinukuu kauli maarufu ya Ataturk, “Siku  moja, mwili wangu utageuka kuwa mavumbi, lakini Jamhuri ya Uturuki itaendelea kuwepo,” Erdogan alisema kauli hiyo inasadifu maono ya mwanzilishi kwa ajili ya taifa imara.

 “Kumuenzi Ataturk inamaanisha kuimarisha jamhuri yetu na kuifanya iwe ya mafanikio katika kila nyanja,” alisema Rais Erdogan.

Ugiriki, alikozaliwa Ataturk

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *