Mkutano huo unaofanyika kwenye mkoa wa Nagara unaopakana na Marekani unatarajiwa kuzungumzia  ufadhili zaidi kwa Ukraine.

Mawaziri hao wanakutana baada ya Rais Donald Trump kuziwekea vikwazo kampuni mbili kubwa kabisa za mafuta za Urusi mwezi uliopita, na kumkosoa vikali Rais Vladimir Putin kwa kukataa kukomesha vita hivyo.

Trump pia ameyashinikiza mataifa ya Ulaya kuacha kununuwa mafuta ya Urusi, akidai kuwa fedha wanazotowa ndizo zinazotumiwa na Moscow kuendeleza vita vyake nchini Ukraine.

Licha ya Kiev kuendelea kukabiliwa vibaya na mashambulizi ya Moscow, Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Kanada, Anita Anand, amejizuwia kuahidi hatua zotote madhubuti kuisaidia Ukraine kwenye mazungumzo hayo ya Niagara.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *