Trump ameipongeza Congo na Rwanda kwa kusaini mkataba wa amani unaosimamiwa na Marekani
Rais Donald Trump aliwapongeza viongozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Rwanda kwa ujasiri wao walipotia saini makubaliano siku ya Alhamisi yenye lengo la kumaliza mzozo wa mashariki mwa Congo na kutoa fursa ya uchimbaji madini kwa Marekani.