Hali hiyo ya wasiwasi nchini humo, inaripotiwa kuzua taharuki miongoni mwa mwananchi, hasa katika miji mikubwa kama Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, Arusha na hata Mbeya, ambapo siku mbili hizi kumeshuhudiwa idadi kubwa ya watu wanaonunua bidhaa mbalimbali kwa ajili ya kuweka ndani, huku wakihofia kutokea kwa vurugu kama za Oktoba 29 baada ya uchaguzi.

Wakati huo huo, Mufti wa Tanzania Abubakar Zubeir, amewataka Waislamu wa nchi hiyo, na waumini wa dini nyengine kutojihusisha na maandamano hayo yaliyopangwa kufanyika Siku ya Uhuru.

Tayari taifa hilo la Afrika Mashariki, ambalo kwa miaka yote lina sifa ya utulivu wa kisiasa, kwa kiasi fulani limegubikwa na hali ya wasiwasi, huku mpasuko mkubwa wa maoni na fikra ukishuhudiwa miongoni mwa wananchi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *