Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon siku ya Jumatatu alitoa wito wa kufanyika mabadiliko ya msingi katika Baraza la Usalama, akionya kuwa shirika hilo liko katika hatari ya “kupoteza umuhimu wake” hadi pale mabadiliko yatafanyika kukabiliana na matumizi mabaya ya kura ya turufu.

“Matatizo ya sasa UN yanatokana na sababu nyingi, lakini makosa ya sasa ya Baraza la Usalama kushindwa kufanya kazi vizuri yanachangia sababu za kushtusha,” Ban alisema wakati wa mkutano wa Baraza la Usalama kujadili majukumu ya mkuu atakayekuja wa Umoja wa Mataifa.

Alisema shughuli za baraza lazima zifanyiwe mabadiliko na kuimarishwa.

Ban aliongeza kuwa baraza hilo kwa muda mrefu limekubwa na “migawanyiko na njama za kutatiza,” lakini “njia mbaya ambazo mataifa mengi sasa wanakiuka majukumu yao zinatia hofu.”

Matumizi mabaya ya kura ya turufu

Alisema kuwa baadhi ya nchi “muda mwingi wanadharau” majukumu ya Umoja wa Mataifa “kupitia matumizi ya kura ya turufu kujikinga wenyewe, washirika wao, na mambo yao kutokana na uwajibikaji.”

Bila mabadiliko muhimu kukabiliana na matumizi mabaya ya kura ya turufu kwa wanachama wa kudumu, kutaleta “kukata tamaa,” Ban alionya, akionya: “Mabadiliko ya Baraza ni magumu lakini ni muhimu na yanawezekana. Bila mabadiliko, Umoja wa Mataifa uko kwenye hatari ya ‘‘kupoteza umuhumi wake.”

Baraza hilo lina nchi wanachama 15, huku kukiwa na wanachama watano wa kudumu, ikiwemo China, Ufaransa, Urusi, Uingereza, na Marekani, na 10 ambao si wanachama wa kudumu wanaoteuliwa kuhudumu kwa kipindi cha miaka miwili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *