Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC) kimefungua kesi katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ), kupinga uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzima huduma za intaneti, kati ya Oktoba 29 na Novemba 4, 2025 nchini humo.

Katika shauri lao, watetezi hao wa haki za kibinadamu, wanadai kuwa uamuzi huo ulikwenda kinyume na katiba ya nchi hiyo ambao pia ulikandamiza haki za msingi za raia.

Waliopo ‘kikaangoni’ katika kesi hiyo, ni pamoja na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini humo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na baadhi ya makampuni ya simu nchini humo.

Walalamikaji hao wanataka uamuzi huo uharimishwe, kuwepo na zuio la maamuzi kama hayo siku zijazo, na kuwepo msahama wa wazi kufuatia tukio hilo.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHRC) kimefungua kesi katika Mahakama ya Haki ya Afrika Mashariki (EACJ), kupinga uamuzi wa serikali ya Tanzania kuzima huduma za intaneti, kati ya Oktoba 29 na Novemba 4, 2025 nchini humo.

Katika shauri lao, watetezi hao wa haki za kibinadamu, wanadai kuwa uamuzi huo ulikwenda kinyume na katiba ya nchi hiyo ambao pia ulikandamiza haki za msingi za raia.

Waliopo ‘kikaangoni’ katika kesi hiyo, ni pamoja na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini humo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na baadhi ya makampuni ya simu nchini humo.

Walalamikaji hao wanataka uamuzi huo uharimishwe, kuwepo na zuio la maamuzi kama hayo siku zijazo, na kuwepo msahama wa wazi kufuatia tukio hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *