Benin imewakamata watu karibu 30, wengi wao wakiwa wanajeshi, kwa madai ya kuhusika na jaribio la mapinduzi lililotibuliwa mwezi huu, vyanzo vya kisheria vimeiambia AFP.

Wanajeshi walijitokeza kwenye televisheni ya taifa Disemba 7 kutangaza kuwa Rais Patrice Talon amepinduliwa lakini jaribio hilo la mapinduzi lilitibuliwa na wanajeshi watiifu.

Watu kadhaa waliuawa na kiongozi wa yaliyodaiwa kuwa mapinduzi, Luteni Kanali Pascal Tigri, na wanajeshi walioasi hawajulikani waliko.

Siku ya Jumatatu, watu karibu 30 wanaoshtumiwa walifikishwa mbele ya mwendesha mashtaka maalum wa mahakama ya uhalifu wa kiuchumi na ugaidi katika mji wa Cotonou, vyanzo vilisema siku ya Jumanne.

Kukamatwa kabla ya kesi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *