Mwenyekiti Baraza la Mpito la Sudan Abdel Fattah al-Burhan yuko tayari kufanya kazi na Rais wa Marekani Donald Trump kwa lengo la kumaliza mgogoro unaogawanya nchi, wizara ya mambo ya nje imesema siku ya Jumanne.

Wizara hiyo ilitoa taarifa hiyo baada mkuu huyo wa majeshi kufanya ziara mjini Riyadh kama mgeni wa Mwanamfalme Mohammed bin Salman, ambaye hivi majuzi aliwasilisha mapendekezo ya amani Sudan kwa Trump katika ziara ya hivi karibuni jijini Washington.

Kulingana na taarifa ya Sudan, Burhan alipongeza “dhamira ya mazungumzo na juhudi za kutafuta na kumaliza vita nchini kwake” za Trump, na kwa ushiriki wa Saudi Arabia.

“Alithibitisha utayari wa Sudan kufanya kazi na Rais Trump, waziri wake wa mambo ya nje, na mjumbe wake kuhusu amani ya Sudan kwa kutimiza lengo hili la msingi,” ilisema, akizungumzia kuhusu Marco Rubio na Mjumbe wa Marekani Massad Boulos.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *