Mashirika ya misaada na Umoja wa Mataifa yamekuwa yakitaka kuwepo kwa njia salama kufikia Al Fasher, ambapo hakuna mawasiliano na maelfu ya walionusurika wamekwama huko, wengi wakiwa wamezuiwa na RSF.

Hakuna thibitisho rasmi la idadi ya waliouawa katika vita vya Sudan vilivyoanza Aprili 2023, huku ikikadiriwa kuwa watu zaidi ya 40,000 wameuawa.

Mkuu wa Baraza la Mpito la Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, anaongoza jeshi huku RSF ikiongozwa na naibu wake wa zamani, Mohamed Hamdan Dagalo.

Mapigano hayo pia yamesababisha mamilioni ya watu kuondoka katika makazi yao, pamoja na kuwepo kwa baa kubwa zaidi la njaa duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *