Hatua hizi zilitangazwa na serikali ya Rais wa Marekani Donald Trump, na zinaweka vikwazo vya usafiri na viza kwa raia wa nchi husika.

Trump pia aliweka vizuizi vya muda vya kusafiri Marekani kwa raia wa nchi zingine za Kiafrika zikiwemo Nigeria, Ivory Coast, Senegal, Angola, Gabon, Gambia, Malawi, Mauritania, Zambia na Zimbabwe.

Kwa Tanzania, hatua hii sio marufuku kamili ya kusafiri kwenda Marekani.

Badala yake, Marekani imeamua kupunguza na kudhibiti baadhi ya aina za viza zinazotolewa kwa Watanzania.

Hii ina maana kwamba bado kuna Watanzania wanaoweza kusafiri kwenda Marekani, lakini njia fulani za kupata viza zimekuwa ngumu zaidi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *