Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ujerumani Alexander Dobrindt amesema wanatarajia kukamilisha mchakato wa kulishughulikia suala hilo mnamo mwezi huu wa Desemba, ili kuwaruhusu watu hao kuwasili nchini Ujerumani. Mpango huo uliidhinishwa na utawala uliopita na Kansela Friedrich Merz aliusitisha mara tu alipoingia madarakani.

Watakaonufaika na mpango huo ni watu walioshirikiana na jeshi la  Ujerumani nchini Afghanistan wakati wa vita dhidi ya Taliban, au wale waliotajwa kuwa katika hatari kubwa baada ya Taliban kurejea madarakani mnamo mwaka 2021, ikiwa ni pamoja na wanaharakati wa haki za binadamu, waandishi wa habari pamoja na familia zao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *