Awali, jumla ya watu 126 walipangwa kurejeshwa nchini, lakini saba walilazimika kuahirisha safari zao dakika za mwisho. Wizara hiyo ilieleza kuwa juhudi zinaendelea kuhakikisha Wakenya waliobaki wanarejeshwa salama, licha ya hali ngumu ya kiusalama na kisiasa katika eneo hilo.

Wizara hiyo ilifafanua kuwa mitandao ya kihalifu imekuwa ikiendesha vituo vya utapeli na kuajiri wafanyakazi kutoka mataifa mbalimbali duniani, wakiwemo Wakenya, mara nyingi kupitia matangazo ya kazi ya uongo.

Kwa sasa, Wakenya 198 wanasubiri kurejeshwa nyumbani. Kati yao, 66 wanazuiliwa katika Kituo cha Uhamiaji cha Thailand, huku 129 wakipewa hifadhi katika makazi ya muda nchini Myanmar.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *