Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIV, katika hotuba yake ya kwanza ya Krismasi aliyoitoa kwenye Kanisa la Mtakatifu Petro na isiyo ya kawaida kwa ibada ambayo wakati wote huwa ya kiroho na tulivu pia amelaani mateso ya watu wasio na makazi duniani na uharibifu unaosababishwa na vita.

Papa Leo amesema maisha ya raia wasio na ulinzi, hususan vijana wanaolazimishwa kubeba silaha, miili yao dhaifu huachwa na majeraha ya kudumu.

Katika ibada hiyo ya ujumbe wa baraka kwa nchi, miji na ulimwengu mzima,  kiongozi wa Kanisa Katoliki, Papa Leo, ametoa mwito wa kukomeshwa vita vinavyondelea kokote duniani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *