#HABARI:Wananchi wameendelea kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro kutambua miili ya ndugu zao, waliopoteza maisha kwenye ajali ya basi na lori, yaliyogongana na kuteketea kwa moto huku tayari mwili mmoja ukitajwa kutambuliwa, licha ya ndugu wengine wakiendelea kutafuta ndugu zao bila mafanikio tangu kuripotiwa kwa ajali hiyo.
Akizungumza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro Kaimu Mganga Mfawidhi Daktari Joseph Kkway, ameeleza kuanza kutambuliwa kwa mwili mmoja huku ndugu waliofika kutambua miili ya jamaa zao akiwemo Bi.Scholastica Yoving akisema tangu wapate taarifa ya ajali hiyo, wamekuwa wakimtafuta mtoto wa dada yake ambae hadi sasa hawajafanikiwa kumuona.
Kwa upande wake mmoja wa majeruhi katika ajali hiyo, Bwana Pelegreen Michael, amesema kuwa alikuwa akisafiri na basi hilo la Mawio, kutoka Morogoro kwenda Tanga, huku mwendo wa gari hilo ukiwa mzuri licha ya kuwepo kwa mvua hadi walipofika eneo la Gwata ndipo wakagongana uso kwa uso na lori.
CP Awadhi Haji ni Mkuu wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini ambaye amefika katika eneo la tukio na kuwajulia hali majeruhi, ambapo amethibitisha kutokea kwa vifo vya watu kumi pamoja na majeruhi ambao amesema baadhi yao kwa sasa wanaendelea vizuri.
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KISHIRIKI MCHEZO SUPA:
–
📱Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M – Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 📱kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania
#Follow @itvtz @radioonetanzania
@capitaldigitaltanzania.