
“Migodi mikubwa imekuwa ikiagiza bidhaa kutoka nje, hata zile zinazopatikana nchini, hali iliyosababisha fedha nyingi kutoka nje ya nchi bila kuzinufaisha Serikali,” alisema Mavunde, akiongeza kuwa hata bidhaa za msingi kama mayai na kuku ziliwahi kuagizwa kutoka nje.
Kwa mujibu wa Serikali ya Tanzania, utekelezaji wa kanuni hizo unalenga kuongeza ajira, kukuza nafasi za uongozi kwa wazawa na kuimarisha mchango wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa.
Katika miaka ya hivi karibuni, Tanzania imechukua hatua kadhaa za kuimarisha sekta hiyo, ikiwemo ujenzi wa viwanda vya kuchakata madini, maabara, pamoja na marekebisho ya baadhi ya sheria zilizokuwa zikionekana kuwa kandamizi kwa wazawa.
Hata hivyo, Serikali inakiri kuwa changamoto kubwa imekuwa kwenye utekelezaji wa sheria hizo.
Wizara ya Madini sasa imetunga kanuni mpya zinazoweka zuio kwa zaidi ya bidhaa 20 kufanywa na wageni, hatua inayolenga kuhakikisha Watanzania wanapata manufaa halisi ya rasilimali za madini zilizopo nchini.