Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, ameshiriki katika mkutano uliofanyika kupitia mtandaoni kilichojadili maandalizi ya awamu ya pili ya mpango wa amani wa Gaza.

Kwa mujibu wa vyanzo vya wizara ya mambo ya nje ya Uturuki, Fidan alijiunga na mkutano huo wa mtandaoni siku ya Jumatatu kama mwendelezo wa mazungumzo yaliyofanyika Miami, Florida, nchini Marekani mwishoni mwa Disemba 2025.

Mkutano huo uliwakutanisha maafisa kutoka Marekani, Misri na Qatar ili kujadili maandalizi ya hatua inayofuata ya mpango wa amani wa Gaza.

Makubaliano ya kusitisha mapigano yalianza kutekelezwa Gaza tarehe 10 Oktoba chini ya mpango wa vipengele 20 wa Rais wa Marekani Donald Trump, hatua iliyosimamisha mashambulizi ya Israel yaliyodumu kwa miaka miwili, ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 70,000—hasa wanawake na watoto—na kujeruhi karibu watu 171,000 tangu Oktoba 2023.

Diplomasia

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *