Donald Trump amepangwa kushiriki katika mkutano kuhusu Greenland na “vyama mbalimbali” leo Jumatano, Januari 21, kando ya Jukwaa la Uchumi la Davos. Kabla ya kuondoka kwenda Uswisi, rais wa Marekani aliahidi “kitu ambacho kitakuwa chanya sana kwa kila mtu” kuhusu matarajio yake kwa Greenland. Siku iliyotangulia, akizungumza katika jukwaa hilo, Emmanuel Macron alilaani nia ya Marekani kutaka kuteka Greenland.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Rais wa Marekani anatarajiwa kuhutubia Jukwaa la Uchumi Duniani huko Davos Jumatano asubuhi baada ya hotuba ya Emmanuel Macron katikati ya mvutano kuhusu Greenland. Siku ya Jumanne, wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House, Rais wa Marekani Donald Trump alisisitiza kwamba Marekani inahitaji Greenland kwa sababu za “usalama wa taifa, na hata usalama wa dunia.” Alitangaza kwamba jambo “chanya sana kwa kila mtu” liko karibu kutokea, hata kama vitisho vyake vya kuiunganisha vinadhoofisha Muungano wa Atlantiki.

Siku ya Jumanne rais wa Marekani alitangaza mkutano kuhusu Greenland na “vyama mbalimbali” kando ya Jukwaa la Uchumi la Davos. “Nimekubali mkutano wa pande mbalimbali huko Davos, Uswisi,” rais wa Marekai aliandika kwenye mtandao wake wa Truth Social, bila kutaja ni lini mkutano huo ungefanyika.

Siku ya Jumanne, katika mkutano wa mtandaoni na mwenzake wa Marekani, Emmanuel Macron alilaani “sheria ya wenye nguvu zaidi” katika Jukwaa la Uchumi wa Dunia huko Davos na akasema anapendelea “heshima kuliko uovu” na “utawala wa sheria kuliko ukatili” kujibu matarajio ya Trump kuhusu Greenland. Rais wa Ufaransa alitaja kutumia chombo cha “kupinga kulazimishwa” cha Umoja wa Ulaya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *