
Rais wa Marekani Donald Trump amezindua “Baraza lake jipya la Amani” na kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky siku ya Alhamisi huko Davos, akijaribu kuimarisha taswira yake kama “mtu anayejitangaza kuwa mpatanishi” baada ya kumaliza mgogoro wa Greenland siku iliyopita—mgogoro ambao yeye mwenyewe alikuwa ameuchochea.
Imechapishwa:
Dakika 3 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Baada ya wiki kadhaa za kauli nzito za uchochezi, rais wa Marekani ghafla alitangaza siku ya Jumatano jioni katika hoteli ya kifahari ya Uswisi Alpine, ambapo anahudhuria mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani, “makubaliano ya kimkakati ya baadaye” kuhusu Greenland. Pia aliondoa vitisho vyake kuhusu ushuru na hatua za kijeshi.
Siku ya Alhamisi, amepangwa kushiriki saa 4:30 asubuhi (saa za Ufaransa) katika sherehe ya kusaini mkataba wa kuanzishwa kwa “Baraza la Amani” chini ya udhibiti wake, linalokusudiwa kufanya kazi ya kutatua migogoro kote ulimwenguni kwa ushindani na Umoja wa Mataifa.
Hapo awali lilibuniwa kusimamia ujenzi mpya wa Gaza. Lakini rasimu ya mkataba inajumuisha agizo pana zaidi kuliko suala la eneo la Palestina tu.
Ada ya kujiunga na Baraza la Amani la Donald Trump ni dola Bilioni kwa kiti cha kudumu
Donald Trump alisema huko Davos kwamba Vladimir Putin alikubali mwaliko huo. Hapo awali, rais wa Urusi alibainisha tu kwamba Wizara yake ya Mambo ya Nje “ilipewa jukumu la kusoma” pendekezo la Marekani.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alitangaza kwamba amekubali kshiriki kwenye baraza la Amani la Donald Trump.
Washirika wakuu wa Marekani, hasa Ufaransa na Uingereza, wameelezea mashaka yao kuhusu “Baraza hili la Amani.” Lakini nchi nyingi za Mashariki ya Kati ziko zimekuali kujiunga na Baraza hilo la Amani, ikiwa ni pamoja na Saudi Arabia na Qatar.
Takriban viongozi 35 tayari wamekubali kujiunga, kati ya mialiko 50 iliyotumwa, afisa mkuu wa utawala wa Trump aliwaambia waandishi wa habari siku ya Jumatano.
“Nadhani hili ndilo baraza bora zaidi kuwahi kuundwa,” alijisifu Donald Trump siku ya Jumatano wakati wa mkutano na mwenzake wa Misri, Abdel Fattah Al Sisi, ambaye ni miongoni mwa wale waliokubali mwaliko huo.
Rais wa Marekani hafichi kujichanganya kwa kutopokea Tuzo ya Amani ya Nobel, licha ya kudai mara kwa mara kwamba amemaliza vita nane, rekodi ambayo inapingwa.
Mkutano na Zelensky
Mwaliko wa Vladimir Putin unasababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa washirika wa Marekani, hasa Ukraine, ambayo inatafuta kukomesha karibu miaka minne ya vita na Urusi, ambayo ilivamia nchi yake mnamo mwezi Februari 2022.
Donald Trump anapanga kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky baada ya uzinduzi wa “Baraza lake la Amani.”
Mjini Davos siku ya Jumatano, alidai kwamba Urusi na Ukraine zitakuwa “wajinga” ikiwa zitashindwa kufikia makubaliano ya kukomesha mzozo huo, ambao aliahidi kuutatua, siku moja baada ya kuchukua madaraka mwaka mmoja uliopita.
Na alirudia kwamba marais wa Urusi na Ukraine walikuwa karibu na makubaliano, dai ambalo amerudia mara nyingi, hata kama amekuwa akimlaumu mmoja au mwingine kwa ukosefu wa kusitisha mapigano.
Kwa muda mrefu akisita kutoa msaada kwa Ukraine, Donald Trump alisema Jumatano huko Davos kwamba ilikuwa juu ya NATO na Ulaya “kushughulika na Ukraine,” sio Marekani.
Hata hivyo, mjumbe wa Marekani Steve Witkoff amepangwa kuondoka Davos kuelekea Moscow siku ya Alhamisi, akiambatana na mkwewe Trump, Jared Kushner, kwa mazungumzo na Vladimir Putin.
Siku ya Jumanne, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alielezea wasiwasi wake kuhusu kupoteza umakini wa kimataifa kuhusu mzozo wa Ukraine, ambao ni wa umwagaji damu zaidi barani Ulaya tangu Vita vya Pili vya Dunia, kutokana na mzozo uliosababishwa na matarajio ya rais wa Marekani ya kuiteka Greenland.
Donald Trump alidai Jumatano kwamba yeye na Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte wamefikia “makubaliano ya kimkakati ya baadaye kuhusu Greenland.”
Bado kuna “kazi nyingi ya kufanya” kufikia makubaliano kuhusu Greenland, Bw. Rutte ameliambia shirika la habari la AFP.