Rais wa Marekani Donald Trump ametoa wito kwa Urusi siku ya Alhamisi kukomesha vita na Ukraine, kufuatia mkutano “mzuri” alioufanya huko Davos na mwenzake wa Ukraine, Volodymyr Zelensky. “Vita lazima viishe,” rais wa Marekani amewaambia waandishi wa habari, ambao walikuwa wakimuuliza ni ujumbe gani alitaka kumtumia Rais wa Urusi Vladimir Putin.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Baada ya kufichua “Baraza lake jipya la Amani,” Donald Trump alikutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky siku  ya Alhamisi, Januari 22, huko Davos, akijaribu kuimarisha taswira yake kama “mtu anayejitangaza kuwa mpatanishi” baada ya kumaliza mgogoro wa Greenland siku iliyopita – mgogoro ambao yeye mwenyewe alikuwa ameanzisha.

Wakati huo huo Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema kwamba Ulaya “imegawanyika” na “imenyweya” mbele ya Donald Trump, akiona kwamba “uungaji mkono wa Rais Trump ni muhimu sana” na kwamba dhamana za usalama zilizopendekezwa na nchi za Ulaya ili kuzuia uvamizi mwingine wa Urusi hazitoshi bila ushiriki wa Marekani. “Kwa mara nyingine tena, kila mtu ana mtazamo chanya, lakini uungwaji mkono wa Rais Trump ni muhimu. Na kwa mara nyingine tena, hakuna dhamana ya usalama inayoweza kufanya kazi bila Marekani,” alisema katika hotuba kali katika Jukwaa la Uchumi Duniani, ambapo alikosoa ukosefu wa “utashi wa kisiasa” wa Ulaya.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky awasili katika Jukwaa la Uchumi Duniani huko Davos, Januari 22, 2026.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky awasili katika Jukwaa la Uchumi Duniani huko Davos, Januari 22, 2026. © AFP – FABRICE COFFRINI

Rais Volodymyr Zelensky alitangaza mazungumzo ya “pande tatu” yaliyopangwa kati ya Ukraine, Marekani, na Urusi katika Falme za Kiarabu.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema kwamba suala la maeneo mashariki mwa Ukraine linalodaiwa na Moscow “halijatatuliwa bado” katika muktadha wa mazungumzo yanayolenga kukomesha vita. “Kila kitu kinazunguka sehemu ya mashariki ya nchi yetu. Kila kitu kinazunguka maeneo.” “Hili ndilo tatizo ambalo hatujatatua bado,” Zelensky alisema katika mkutano na waandishi wa habari pembezoni mwa Jukwaa la Uchumi la Davos.

Mkutano huko Davos kati ya kiongozi wa Ukraine Volodymyr Zelensky na Rais wa Marekani Donald Trump ulianza saa sita mchana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *