
Kocha wa Senegal Pape Thiaw amefungiwa mechi tano na kupigwa faini ya dola za kimarekani 100,000 kwa kile ambacho CAF imesema alifanya mambo kinyume na utaratibu na kuuchafua mchezo huo ambao timu yake ya Senegal ilishinda 1-0 baada ya muda wa ziada.
Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) nalo limetozwa faini ya jumla ya dola 615,000 kwa makosa mbalimbali wakati wa mchezo huo.
AFCON 2025 Morocco kadhalika imeadhibiwa kwa kupigwa jumla ya faini ya dola za kimarekani 315,000 kwa makosa, wakati wa mchezo huo wa fainali.