Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar imesema hayo jana Jumatatu baada ya kuongoza mazungumzo mjini Doha na kuongeza kuwa timu hiyo itapelekwa Uvira, mji wa kimkakati mashariki mwa Kongo, ambao waasi hao waliudhibiti mwezi Disemba.

Tangazo hilo lililotolewa jana usiku ni ishara ya kupigwa hatua katika mazungumzo ya moja kwa moja yaliyoratibiwa na Doha kati ya Congo na AFC/M23, ambao mwaka uliopita walidhibiti ardhi kubwa kabisa kuwahi kuikamata Mashariki mwa taifa hilo.  

Msukumo huu wa karibuni wa kufanyia tathmini usitishwaji wa mapigano hata hivyo, unafanyika wakati mapigano yakiendelea kwenye eneo hilo la mashariki.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *