
Iran na Marekani zimekubaliana “kuendelea na mazungumzo yao,” Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi ametangaza siku ya Ijumaa baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo yaliyofanyika Oman, ambayo aliyaelezea kuwa na mazingira “chanya”.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mazungumzo haya yasiyo ya moja kwa moja yamefanyika wakati kikosi kikubwa cha majini cha Marekani kilipopelekwa katika Ghuba, huku Donald Trump akizidisha vitisho vyake vya kuingilia kijeshi nchini Iran kufuatia ukandamizaji mkali wa utawala wa Iran dhidi ya maandamano yaliyoenea mapema mwezi Januari.
“Katika mazingira chanya, mawazo yetu yalibadilishwa na maoni ya upande mwingine yaliwasilishwa kwetu,” Araghchi ameiambia televisheni ya taifa ya Iran. Ameongeza kuwa pande zote mbili “zimekubali kuendelea na mazungumzo, lakini taratibu na ratiba zitaamuliwa baadaye.” “Hatua zinazofuata zitategemea mashauriano yetu na serikali zetu,” amesema, pia akielezea matumaini kwamba Washington ingejiepusha na “vitisho na shinikizo” ili “mazungumzo yaweze kuendelea.” Ameongeza pia, kulingana na shirika rasmi la habari la IRNA, kwamba majadiliano hayo yanalenga “pekee suala la nyuklia.” “Hatujadili mada nyingine yoyote na Marekani,” amesema.
Vikwazo vipya vya mafuta dhidi ya Iran
Marekani imetangaza vikwazo vipya vya mafuta dhidi ya Iran saa chache tu baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo huko Oman, yaliyofanyika katika “mazingira chanya,” kulingana na Tehran. Vikwazo hivi vinalenga makampuni 15, watu wawili, na meli 14 zinazohusishwa na biashara haramu ya mafuta ya Iran na bidhaa za petroli, kulingana na taarifa yaWizara ya Mambo ya Nje.
Wakati Washington ikidai majadiliano si tu kuhusu suala la nyuklia bali pia kuhusu uungaji mkono wa Iran kwa makundi mbalimbali yenye silaha yanayoipinga Israel na mpango wake wa makombora ya masafa marefu, Tehran inabainisha kwamba inataka tu kushughulikia suala la nyuklia ili kuhakikisha kuondolewa kwa vikwazo vya kimataifa vinavyodhoofisha uchumi wake. Mazungumzo haya yasiyo ya moja kwa moja yalmeanyika wakati kikosi kikubwa cha majini cha Marekani kilipopelekwa Ghuba, huku Donald Trump akizidisha vitisho vyake vya kuingilia kijeshi nchini Iran kufuatia ukandamizaji wa umwagaji damu wa utawala wa Iran dhidi ya maandamano makubwa mapema mwezi Januari.