• Aliyekuwa Afisa wa Gereza Shakur alijiunga na mkutano wa ODM wa Linda Mwananchi mjini Busia, na kuapa kuchukua hatua kali iwapo upinzani utashinda 2027
  • Katibu Mkuu Edwin Sifuna alizindua ziara hiyo huko Busia, akitaja ngome kubwa ya wapiga kura wa ODM kaunti hiyo na kuahidi uongozi usioyumba
  • Sifuna alikosoa chama tawala cha UDA kwa kukosa kutekeleza makubaliano yoyote na ODM na kuonya dhidi ya jaribio lolote la ODM

Aliyekuwa afisa wa gereza Jackson Kuria Kihara, almaarufu Cop Shakur, alihudhuria maandamano ya Orange Democratic Movement (ODM) huko Busia Jumapili, Februari 8.

askari
Askari Shakur aliapa kumfunga jela Rais William Ruto iwapo upinzani utajinyakulia ushindi katika uchaguzi wa 2027. Picha: Mpasho, William Ruto.
Source: Facebook

Hafla hiyo ya Linda Mwananchi iliandaliwa na mrengo wa chama hicho ukiongozwa na Katibu Mkuu Edwin Sifuna, gavana wa Siaya James Orengo na Mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino.

Shakur, ambaye amekamatwa mara kadhaa kutokana na uharakati wake mtandaoni ikiwa ni pamoja na mashtaka ya kuchapisha habari za uongo na uchochezi wa uasi, alisema alimkabili Rais William Ruto kwa ujasiri wakati wa maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha wa 2024.

Pia soma

James Orengo, Edwin Sifuna na Babu Owino Waanza Ziara ya Linda Mwananchi Masaibu ya ODM Yakizidi

Je, Ruto atafungwa jela ikiwa upinzani utashinda 2027?

“Mimi ndiye afisa niliyemwambia Ruto akome kuwaua vijana,” aliambia umati.

Aliapa kwamba ikiwa upinzani utachukua mamlaka 2027, Ruto atafungwa katika Gereza la Kamiti Maximum. “Nataka tuungane kama vijana, na kumpeleka Ruto nyumbani 2027. Na tukitwaa mamlaka, Ruto atafungwa Kamiti. Je, aende au asiende?” aliuliza, huku akishangiliwa

Ni kaunti gani ambayo wanachama wengi wa ODM wamejiandikisha kuwa wapiga kura?

Sifuna alieleza ni kwa nini ziara hiyo ilianza Busia, akibainisha kuwa kaunti hiyo ina idadi kubwa zaidi ya wapiga kura waliosajiliwa wa ODM, kupita kaunti za kando ya ziwa ambazo zilikuwa ngome ya kiongozi wa zamani Raila Odinga.

“Kama katibu mkuu wa ODM, nasema kwamba kaunti iliyo na asilimia kubwa ya wapiga kura waliojiandikisha ambao ni wanachama wa ODM si Siaya, si Homa Bay, si Migori, ni Busia. Na ndio maana tuliamua kuzindua ziara hii ya Linda Mwananchi hapa. Nataka unipe maagizo kama wakuu wangu wa ODM, je, tuendelee na njia hii au la?”

Pia soma

Magazeti ya Kenya: Wakenya walioajiriwa na jeshi la Urusi kutokea Qatar wauawa Ukraine

Aliapa kwamba atabaki imara katika kutetea kanuni za chama.

“Nataka kuapa mbele ya Mungu na mbele yenu kama wakubwa wangu, sitayumba kutoka kwenye nafasi yangu. Baba (Raila) hakuwashauri waoga. Hata kama itamaanisha kutuua, iwe hivyo. Lakini tutaendelea kusema ukweli kila siku,” aliongeza.

Sifuna alisema haogopi kifo, akidai watu wa Busia wanajua nyumbani kwake na wako tayari kumzika ikibidi.

Alikosoa maswala kama vile kucheleweshwa kwa wanafunzi wa shule, masaibu ya vyuo vikuu, na changamoto zingine za kijamii.

Je, Sifuna alisema nini kwenye ajenda ya pointi 10 za ODM-UDA?

Akizungumzia makubaliano ya vipengele 10 vya ODM-UDA, alisema makataa ya utekelezaji yanakaribia huku zikiwa zimesalia chini ya siku 30, lakini ni kidogo sana zimefanyika.

Alionya kuwa majaribio yoyote ya kuongeza mkataba huo hayatakuwa na maana yoyote.

“Mkataba huo haukuwa wa kubuni muungano na UDA. Una saini mbili pekee, moja ya Ruto na nyingine ya Raila. Nataka kusema hapa kama wakili, hatukutoa nyongeza yoyote ya hati hiyo. Ikiwa kuna mtu ana ndoto ya kurefusha mkataba huo, waende kwenye kaburi la Raila huko Bondo kutafuta sawa,” alisema.

Pia soma

Mazishi ya Raila Odinga: Sifuna ana machungu jeneza la kinara wa ODM halikupambwa rangi za chungwa

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *