Iran na Urusi zitafanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi katika Ghuba ya Oman, huku mvutano na Marekani ukifikia kilele.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Na: RFI na mashirika mengine

Matangazo ya kibiashara

Ingawa Iran imezungumza na Marekani kuhusu mpango wake wa nyuklia nchini Uswisi, Tehran na mshirika wake wa Urusi watafanya luteka ya kijeshi nje ya pwani ya Jamhuri ya Kiislamu siku ya Alhamisi, shirika la habari la ISNA limetangaza leo Jumatano, Februari 18. “Mazoezi haya ya pamoja ya majini” yatafanyika katika Ghuba ya Oman na kaskazini mwa Bahari ya Hindi, ISNA imeripoti, ikimnukuu Admiral Hassan Maghsoudloo.

“Lengo ni kuimarisha usalama wa baharini (katika eneo hili) pamoja na uhusiano kati ya wanajeshi wa majini wa nchi hizo mbili,” shirika hilo limeongeza, bila kutaja muda wa mazoezi. Hii inakuja huku mazoezi mengine ya kijeshi yakianza Jumatatu chini ya usimamizi wa Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), jeshi la kiitikadi la Iran, katika Mlango-Bahari wa kimkakati wa Hormuz.

Tishio la kuzuia Mlango-Bahari

Maafisa wa Iran wametishia mara kwa mara kuzuia Mlango-Bahari huu, hasa wakati wa mvutano na Marekani. Hata hivyo, tishio hili halijawahi kutekelezwa. Njia muhimu ya usafirishaji duniani wa mafuta na gesi asilia iliyoyeyushwa, imekuwa eneo la matukio kadhaa hapo awali na imerejea kwenye uangalizi kutokana na mvutano kati ya Iran na Marekani. Ilifungwa kwa kiasi fulani kwa saa chache siku ya Jumanne kwa sababu za “usalama” wakati wa mazoezi ya kijeshi yanayoendelea, kulingana na televisheni ya serikali ya Iran.

Soma piaIran yaanza luteka ya kijeshi katika Mlango-Bahari wa Hormuz katikati ya mazungumzo na Marekani

Kwa upande wake, Marekani imetuma kikosi kikubwa cha majini katika Ghuba, na kuibua hofu ya kuingilia kijeshi dhidi ya Iran ikiwa mahasimu hao wawili watashindwa kufikia makubaliano, hasa kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran. Walianza tena mazungumzo mapema mwezi Februari, chini ya upatanishi wa Sultan wa Oman, kwa mara ya kwanza tangu vita vya siku 12 vilivyoanzishwa mwezi Juni 2025 na Israel na ambapo Marekani ilijiunga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *