Katambi: Tanzania amani kwanzaKatambi: Tanzania amani kwanza

SHINYANGA: WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amesema Tanzania itaendelea kuwa na amani na utulivu huku akiwaonya watu wanaotumika kuichafua nchi na kuzua taharuki kwa kupewa rushwa.

Waziri huyo ambaye ni mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini amesema hayo leo alipokuwa kwenye mkutano wa hadhara aliouandaa kuwashukuru wananchi kumpa ridhaa ya kuwa mbunge tena na kumshukuru Rais kumchagua kwenye nafasi hiyo kumwakilisha.

Katambi amesema watumishi wa serikali ambao wazembe mwisho wake umefika kwani fedha zimekuwa zikitolewa na serikali za utekelezaji miradi lakini wanachelewesha kwa uzembe wao hivyo hatua kali zitachukuliwa.

“Ninaomba nipewe ruhusa nishughulikie watumishi wa umma wa serikali na wakandarasi wazembe nianze kuwaondoa nanipambane na tatizo la rushwa na kusimamia haki”amesema Katambi.

Katambi amesema wananchi wa mjini Shinyanga wameendelea Kumwamini hivyo atahakikisha maendeleo yanapatikana kwa kasi kubwa kwani serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imetoa zaidi ya Sh Bilioni 45 kwaajili ya ujenzi wa uwanja wa Ndege uliopo Ibadakuli.

Katambi amesema changamoto zote zilizopo ndani ya Manispaa hii kwa kushirikiana na madiwani wataziondoa sanjari na makundi ya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu katika siku 100 za uongozi wa Rais Samia Sh milioni 490 zimetolewa kwenye vikundi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga Janeti Magomi amesema hali ya ulinzi na usalama ni shwari hivyo watahakikisha ulinzi unaimarika kila siku na wananchi waishi kwa usalama na utulivu .

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa amesema wanafuraha kubwa na imani kwa serikali ya awamu hii ila alimuomba Waziri Katambi suala la vitambulisho vya taifa (NIDA) liendelee kwenye kata ili kuwaondolea usumbufu ambao wanafikisha umri wa miaka 18 kuliko kubaki huduma hiyo kutolea ngazi ya wilaya pekee.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *